Tuesday, February 12, 2013

Wanakwenda wapi wakifeli kidato cha nne?





Mwananchi, Jumanne, Februari5  2013

MWAKA 2011, nchi ilishuhudia idadi kubwa ya wanafunzi wakifeli mtihani wa kidato cha nne kwa kupata daraja sifuri.Kwa mujibu wa kumbukumbu za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, watahiniwa 156,089  sawa na asilimia 46.41ya wahitimu wote walifeli mtihani huo kwa kupata daraja hilo la mwisho.Katika mtihani huo wanafunzi 33,577 pekee sawa na asilimia 9.98 ndio waliopata kuanzia daraja la kwanza hadi la tatu, hivyo kuwa na uhakika wa kuendelea na kidato cha tano.

Kwa mujibu wa mfumo wa elimu nchini, wanaopata daraja la nne, baadhi wako shakani kuendelea na daraja la sekondari ya juu. Katika matokeo hayo, hawa walikuwa 146,639 sawa na asilimia 43.60.Ili kujiunga na kidato cha tano, wanafunzi hawa wanapaswa kuwa na alama C katika masomo yasiyopungua matatu.
Aidha, kwa waliopata daraja sifuri ni sawa na kusema miaka minne ya kuwa shule, wameambulia patupu, kwani kwa mfumo uliopo wa elimu hawawezi kuendelea kusoma, labda warudie mitihani au wajiunge na vyuo vinavyopokea wahitimu wa darasa la saba.
Bila shaka jeshi hili la vijana waliofeli ni kubwa, na kwa kuwa nchi haina utaratibu wa kuwaendeleza, swali kuu ni je, wahitimu hawa wanakwenda wapi, wana sifa ya kuajiriwa au hata kuwa na uwezo wa kujiajiri? Kwa habari zaidi bofya hapa.

No comments:

Post a Comment